
Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari
Kibosho, Mhandisi Aloyce Peter Mushi akizungumza wakati wa hafla ya
mahafali ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari ya Kibosho. Kushoto
ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB,
Dk. Charles Kimei akizindua jengo la mahabara ya Shule ya Sekondari
Kibosho, wakati wa mahafali ya 30 ya kidato cha sita yaliyofanyika
Mkoani Kilimanjaro. Kushoto ni Mkuu wa Shule hiyo, sista Anna na kulia
ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo, Mhandisi Aloyce Peter Mushi. Benki
ya CRDB ilitoa mchango wa shs. milioni 5 kwa ajili ya shule hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk.
Charles Kimei akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya
Shule, Mhandisi Aloyce Peter Mushi. Kulia ni Mkuu wa Shule hiyo, Sista
Anna.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk.
Charles Kimei akizindua gazeti la shule. Kushoto ni Mkuu wa Shule ya
Sekondari ya Wasichana ya Kibosho, Sista Anna na Mwenyekiti wa Bodi ya
Shule, Mhandisi Aloyce Peter Mushi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei akitoa zawadi kwa mwanafunzi aliyefanya vizuri katika masomo yake.
source: dullonet.com
No comments:
Post a Comment