Marmo Advert Banner

Royal Tughimbe Hotel

investment forum

investment forum

MACHEMBA STORE

MACHEMBA STORE

MBEYA SPRING WATER

MBEYA SPRING WATER

MADARAKA AUTO GARAGE

MADARAKA AUTO GARAGE

Tuesday, 6 May 2014

KAMPENI MPYA YA JIHUDUMIE YA NMB YAZINDULIWA NCHINI
Benki ya NMB imezindua Kampeni mpya ya JIHUDUMIE lenye lengo la kuwezesha upatikanaji wa haraka wa huduma mbali mbali za Benki hiyo. Akizindua Kampeni hiyo jijini Dar es Salaam Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bwana Mark Wiessing alisema mbali ya upatikanaji wa huduma ya haraka, Kampeni hiyo itawezesha huduma kupatikana muda wowote na mahali popote mteja atakapohitaji huduma hiyo.
Sasa wateja wa NMB wanaweza kupata huduma bila kwenda katika tawi la NMB. “Tunapenda kuwafahamisha wateja wetu kwamba sasa wanaweza kupata huduma za kibenki kupitia simu za mkononi na njia nyingine mbadala kama mashine za ATM, huduma za benki kwa njia ya intaneti, PesaFasta na Akaunti ya Chap Chap,” alisema Wiessing.
Kupitia kampeni hiyo, NMB imeweza kuzingatia mahitaji ya msingi ya wateja wake, ikiwemo uhakika wa huduma za kibenki na uwezo wa kuzipata wakati wowote na mahala popote. 
“Kwa kubonyeza tu kitufe cha simu, fedha itaweza kutoka kwenye akaunti yako ya NMB kwenda mahala pengine popote kama vile kwenye malipo ya LUKU, kulipia muda wa maongezi wa simu na hata kuweza kutoa kiasi kinachofikia shilingi milioni moja kupitia mashine za ATM,” alisema.
Baada ya uzinduzi huo mwendelezo ulifanywa kwa matawi yote ya benki hiyo jijini Dar es Salaam, wateja wa benki hiyo walisifia kampeni hiyo, wakisema imelenga kuwapunguzia adha, usumbufu na kuokoa muda wa kupata huduma za kibenki.

Afisa Mkuu wa Huduma kwa Wateja Wakubwa wa NMB Bw. Richard Makungwa akiwapa maelezo wateja kuhusu huduma wa Jihudumie katika tawi la NMB Magomeni.
Afisa Mkuu wa Ukaguzi wa ndani wa benki ya NMB Bw. Augustino Mbogella (Kulia) akielimisha wateja katika tawi la NMB Sinza kuhusu huduma za jihudumie ambazo ni, NMB mobile, PesaFasta, NMB ATM, NMB ChapChap account, POS, NMB Tigo Pesa, NMB M-Pesa na NMB inakubalika hapa
Afisa Mkuu wa Benki ya NMB Bwana Waziri Barnabas (Kushoto) akimpatia maelekezo ya namna ya kutumia huduma ya kifedha ya JIHUDUMIE mteja Bwana Francis Mbena katika tawi la Kariakoo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo

No comments: