Marmo Advert Banner

Royal Tughimbe Hotel

investment forum

investment forum

MACHEMBA STORE

MACHEMBA STORE

MBEYA SPRING WATER

MBEYA SPRING WATER

MADARAKA AUTO GARAGE

MADARAKA AUTO GARAGE

Tuesday, 15 April 2014

TAARIFA YA MAENDELEO YA UJENZI WA VITUO VYA UTOAJI WA HUDUMA KWA PAMOJA MIPAKANI (ONE -STOP BOARDER POSTS)

Msururu wa magari katika mpaka wa Tunduma, Mbeya. Hali hii inaashiria mahitaji makubwa ya kuwepo kwa huduma ya pamoja mpakani (One-Stop Boarder Post) ili kuondoa adha kwa wafanyabiashara wa usafirishaji. 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Vedastina Justinian (kati kati) akizungumza na waandishi jana jijini Dar es Salaam kuhusu mradi wa Vituo vya Utoaji Huduma kwa Pamoja Mipakani (One-Stop Boarder Posts) unaolenga kurahisisha taratibu za huduma za forodha, uhamiaji, usimamizi wa ubora wa bidhaa, ulinzi na usalama.
Mradi wa Vituo vya utoaji wa Huduma kwa Pamoja Mipakani (One-Stop Boarder Posts) unatarajiwa kurahisisha huduma mbali mbali zitolewazo mipakani ambazo ni kama vile forodha, uhamiaji, usimamizi wa ubora wa bidhaa, na ulinzi na usalama na kuzitoa upande mmoja tu wa mpaka kwa pamoja. Mradi huu umekwishakamilika kwa baadhi ya mipaka hapa nchini kama vile Holili, Mutukula na Sirari. Ujenzi wa Vituo vingine kama vile Namanga, Horohoro na Rusumo uko katika hatua za mwisho. Baada ya hapo Mradi huu utaendelea katika maendeleo mengine ya Mipaka kama vile Tunduma.

No comments: