Marmo Advert Banner

Royal Tughimbe Hotel

investment forum

investment forum

MACHEMBA STORE

MACHEMBA STORE

MBEYA SPRING WATER

MBEYA SPRING WATER

MADARAKA AUTO GARAGE

MADARAKA AUTO GARAGE

Saturday, 29 March 2014

KAMPUNI KUBWA ZA UJENZI ZA UTURUKI ZAVUTIWA KUFANYA KAZI TANZANIA

Kampuni kadhaa kutoka nchi ya Uturuki zimeanza kuingia Tanzania ili kushiriki katika kazi za ujenzi kwenye maeneo mbali mbali hapa nchini. Kukua kwa sekta ya ujenzi kumekua ndiyo kivutio kikuu kilichozifanya kampuni hizo kuonesha nia ya kufungua ofisi zao hapa nchini.

 Wakizungumza katika kikao na Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli walipomtembelea ofisini kwake, wawakilishi kutoka Kampuni  tatu tofauti wamempongeza Waziri huyo kwa jinsi anavyosimamia sekta hiyo ya ujenzi kiasi cha kuanza kuvutia makampuni makubwa kutoka nje.

 “Tumekuwa tukifuatilia uendeshwaji na ukuaji wa sekta ya ujenzi katika mataifa kadhaa barani Afrika na tumejiridhisha kuwa Tanzania ni nchi inayofanya vizuri katika upande huo” alibainisha Bw. Orhan Babaoglu ambaye ni Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya KAYA ya Uturuki.

 Mwakilishi mwingine kutoka Kampuni ya CEYTUN ya huko huko Uturuki Bw. Kursat Durak amebainisha kuwa, utendaji wa kampuni za Kituruki unafahamika duniani kote, hivyo ujio wao  una lengo la kuamsha ushindani wa ubora lakini pia kuona kuwa gharama za utekelezaji wa miradi hiyo zinathibitiwa kwa kuwa na washindani kutoka maeneo tofauti.

 Mhe. Magufuli kwa upande wake wakati akiwakaribisha amewataka kuzingatia sheria na taratibu zinaoongoza shughuli za kandarasi hapa nchini. 

Waziri Magufuli aliwajulisha kuwa, mbali na kazi za kawaida za kandarasi kwa hivi sasa kuna miradi kadhaa mikubwa ya kiuwekezaji inayokusudiwa kuendeshwa kwa kushirikisha sekta binafsi hivyo hiyo pia ni fursa wanayoweza kujishughulisha nayo hapa nchini.

Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipitia baadhi ya nyaraka zilizowasilishwa na makampuni ya kandarasi kutoka Uturuki. Wengine katika picha (kutoka kulia) ni Naibu Katibu Mkuu Eng. Joseph Nyamhanga, Katibu Mkuu Alhaj Mussa Iyombe na kushoto kabisa ni Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya KAYA Bw. Orhan Babaoglu 
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya KAYA Bw. Orhan Babaoglu (kushoto) akiwasilisha kwa Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, utambulisho wa makampuni ya Uturuki ambayo yamefungua ofisi hapa nchini kwa lengo la kushiriki katika kazi za kandarasi za ujenzi hapa nchini.





  

No comments: