Marmo Advert Banner

Royal Tughimbe Hotel

investment forum

investment forum

MACHEMBA STORE

MACHEMBA STORE

MBEYA SPRING WATER

MBEYA SPRING WATER

MADARAKA AUTO GARAGE

MADARAKA AUTO GARAGE

Saturday, 22 March 2014



UKANDA WA NYANDA ZA JUU KUSINI WAVUTIA WAWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA UTALII NA MIFUGO 



Meneja Kituo Cha Uwekezaji Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Ndugu Daudi Riganda akitoa maelezo juu yakukua kwa sekta ya uwekezaji katika Ukanda huo




Na Emanuel Madafa, Mbeya


HALI ya uwekezaji kwa Mikoa ya Nyanda za juu Kusini, imetajwa kuridhisha kulingana na sekta mbalimbali ambazo zinampa fursa mwekezaji   kuamua kuwekeza eneo  analo lihitaji ikilinganishwa na kipindi cha nyuma kuanzia  mwaka 2008.

Hayo yamesemwa na Meneja wa uwekezaji Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Daud Liganda, ambapo amedai kuwa idadi ya miradi iliyosajiliwa na kituo  hicho imeendelea kukua hasa katika sekta ya kilimo na ufugaji.

Amesema licha ya ukuaji huo kwa kasi    lakini bado    umekuwa hauendani na hali halisi ya maeneo husika hasa kutokana na kuwepo kwa mazingira mazuri ya kiuwekezaji ambayo kama yakitumiwa vyema ukuaji huo utazidi kukuwa kwa kiwango kizuri zaidi ukilinganishwa na kipindi hicho cha miaka mitano iliyopita. .

Amesema katika ukanda huo kuna ardhi  ya kutosha na yenye rutuba  nzuri pamoja na mvua za mara kwa mara zenye uwezo  mkubwa wa kustawisha mazao ya aina yote.

Aidha Meneja huyo amedai kuwa licha ya sekta za kilimo na ufugaji kukuwa kwa kiwango kizuri pia Sekta ya Utalii nayo imezidi kupanda  hasa katika ongezeko la  ujenzi wa hoteli za kisasa zenye hadhi ya kimataifa.

Pamoja na ongezeko hilo pia  meneja huyo amewataka wafanyabiashara wa ukanda huo hasa kwa mkoa wa mbeya kuhakikisha wanaendana na uwepo wa uwanja wa kimataifa wa Songwe ambao umetoa fursa kubwa hasa katika sekta ya utalii.

Ametaja fursa nyingine iliyopo katika mkoa wa mbeya ni ya utoaji wa huduma za kijamii kama vile elimu na afya.  

Amesema bado kituo hicho kinatoa rai kwa wadau mbalimbali katika ukanda huo kuendelea kuchangamkia fursa hizo ili kuweze kuendana na hali halisi ya ukuaji katika nyanja ya kiuwekezaji katika ukanda huo.

Mwisho
 

1 comment:

Anonymous said...

Nina pongeza juhudi za Ndugu Daud ambazo ni za makusudi kabisa za kuwataka watanzania na hasa wafanya biashara wadogo na wakubwa wa mkoa wa Mbeya kuanza sasa kuchukua hatua za kuwekeza badala ya kufanya biashara pekee wakiwa hawana dira . Lakini wakati ndugu Daud anataka watanzania wa Mbeya kwenda hatua zaidi mbele na kuanza kuwekeza nashauri pia TIC waje na mpango shirikishi wa watu hawa wachanga katika mitaji .

Nashauri ndugu Daud atoke ofisini na kufanya maongezi na hawa watu uso kwa uso na awaeleze TIC Kanda inaweza kuwasaidia vipi kufikia malengo kwa ushirikiano .Mimi ninadhani wafanya biashara wadogo wadogo wakiwa na uelewa wa kutosha wanaweza kuwa rafiki mkubwa wa TIC . Lazima wajue kwamba TIC ina faida kubwa kwa wao na si kudhania kwamba ni kwa wageni pekee . Ndugu Daud nakupongeza kwa wito wako na kwa kuona kwamba ni wakati sasa wa mtanzania kipato cha kati kuwa mwekezaji na kushirikiana na TIC na kwa njia hiyo pia ajira itaongezeka Uchumi wa Nchi na hata kipato cha mtu mmojo mmoja kupitia uwekezaji mdogo mdogo.

Chukua hatua watembee na wakaribishe tengeneza familia ya TIC na iwe mfano kwa wengine .
Haya ndiyo maoni yangu kuhusiana na wito wako .