Meneja wa kituo cha uwekezaji Tanzania, kanda ya nyanda za juu kusini bwana Daudi Liganda atoa wito kwa wawekezaji kutumia fursa za uwekezaji mkoani Mbeya ipasavyo.
Akizungumza na blog ya dailybusinesstz, amewaasa wafanyabiashara na wawekezaji kuzitumia fursa zilizoko mkoani Mbeya katika kuongeza faida katika biashara zao.
Bwana David Liganda
Meneja huyo amezitaja fursa hizo kuwa ni, kilimo cha biashara, uanzishaji wa viwanda, ujenzi wa mahoteli na nyumba za biashara, biashara ya usafirishaji, huduma za jamii kama elimu na afya, pamoja na uanzishaji wa vituo vya radio na televisheni.
Aidha amesema, endapo wafanyabiashra hao watajisajili na kituo cha uwekezaji, wanaweza kufaidika kwa kupewa punguzo la kodi katika vifaa watakavyovinunua kwa ajili ya miradi mbalimbali.
Hivyo basi kwa kufanya hivyo wanaweza kuokoa gharama kubwa ambayo ingetumika wakati wa kufanya biashara hizo.
wawekezaji hasa wa ndani wanashauriwa kuitumia ofisi ya kituo cha uwekezaji nyanda za juu kusini kuweza kuendeleza biashara na miradi yao. ofisi hizo zinapatikana katika barabara ya Karume katika jengo la NBC linalotizamana na uwanja wa Sokoine.
No comments:
Post a Comment